Beki wa kulia wa Liverpool Trent Alexander Arnold anafukuzia rekodi inayoshikiliwa na Mesut Ozil wa Arsenal katika Ligi Kuu nchini Uingereza.
Mpaka sasa Trent Alexander Arnold amefanikiwa ku-assist kwenye mechi tano mfululizo za ligi kuu, akifanya hivyo mara ya mwisho dhidi ya Norwich katika ushindi wa 4-1 akimpa assist Divock Origi.
Record ya assist nyingi mfululizo inashikiliwa na Mesut Ozil, ambae ana rekodi ya ku-assist mara 7 mfululizo. Inategemewa Arnold atakaribia kuifikia rekodi hiyo kwenye mechi ijayo ya Liverpool dhidi ya Southampton.
