Ujumbe wa kwanza wa Sugu baada ya kufunga ndoa na mkewe Happiness, "Sasa ni rasmi"



Mbunge wa Mbeya Mjini Joseph Mbilinyi maarufu kama Sugu, ameandika ujumbe wake wa kwanza kwenye mtandao wa Instagram tangu alipofunga ndoa leo (Jumamosi) mchana.

Kupitia mtandao huo Sugu ameweeka picha hiyo hapo juu na kuandika, "Mr & Mrs Joseph Mbilinyi... Sasa ni RASMI zaidi ❤️❤️... #JONGWE#MVMP."

Ndoa ya Sugu na mkewe Happiness Msonga imefanyika katika kanisa la Katoliki Ruanda.