https://monetag.com/?ref_id=TTIb Waziri wa zamani wa Mambo ya Nje "Kaduma" afariki dunia | Muungwana BLOG

Waziri wa zamani wa Mambo ya Nje "Kaduma" afariki dunia


Waziri wa Mambo ya Nje wa zamani katika serikali ya awamu ya kwanza, Ibrahim Kaduma, 82, amefariki dunia nchini India usiku wa kuamkia leo, Jumamosi.

Waziri huyo wa zamani amedaiwa kuwa alienda India wiki iliyopita kwa ajili ya uchunguzi wa afya yake kabla ya umauti kumfika.

Enzi wa uhai wake, Kaduma alikuwa miongoni mwa wanasiasa mashuhuri aliwahi kuhudumu katika serikali kama katibu mkuu katika wizara mbalimbali ikiwemo nafasi ya Waziri wa Mambo ya Nje kuanzia mwaka 1975 hadi 1976.

Mchumi na mwanasiasa huyo  alizaliwa mwaka 1937 huko Mtwango, mkoani Njombe na alifamikiwa kupata elimu yake ya juu katika Chuo Kikuu cha Makerere nchini Uganda na University of York kilichopo Uingereza. Marehemu ameacha mjane, watoto watano na wajukuu tisa.
Tukiwa kama Muungwana Blog tunatoa pole kwa familia ya marehemu na Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi....Amiina.