Wanamgambo saba wa Al-Shabab wauawa leo


Wanamgambo saba wa al-Shabab wameuawa leo katika mapigano makali na vikosi vya serikali ya Somalia katika mkoa wa kusini wa Shabelle ya chini.

Afisa mwandamizi, ambaye alikataa kutajwa jina, ameeleza kwamba mapigano hayo yalizuka baada ya wanamgambo kushambulia kituo chao cha jeshi katika mji mpya wa Awdheegle uliokolewa katika eneo la Chini la Shabelle.

"Wanamgambo waliendesha gari lao karibu na kituo cha jeshi na kulipua mabomu kwenye gari na muda mfupi baadaye vita kali vilitokea. Tuliwauwa wanamgambo saba na kujeruhi wengine 10," afisa huyo alisema.

Wanajeshi wanne walipata majeraha wakati wa shambulio ambalo lilikuja ghafla wiki moja baada ya vikosi vya Somalia kukomboa mji mkakati wa Awdheegle, ambao ulikuwa chini ya simamizi wa al-Shaba