Azam FC wakubali kichapo nyumbani Kombe la Shirikisho Afrika


Azam FC katika mchezo wa Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Triangle United wamepoteza kwa kukubali kufungwa goli 1 kwa bila.

Bao pekee la Triangel United ya Zimbabwe lilifungwa dakika ya 34 na Ralph Kawondera kutokana na uzembe wa safu ya ulinzi wa Azam FC.

Licha ya Azam FC kupewa sapoti kubwa na mashabiki waliojitokeza uwanja wa Azam Complex hayakuzaa matunda kwani safu ya ulinzi ya Triangle United ilikuwa ngumu na ikajilinda na hatari zote.

Sasa Azam FC ina kazi nzito ya kwenda kutafuta matokeo ugenini kwenye mchezo wa marudiano unaoatarajiwa kuchezwa kati ya Septemba 27-29 nchini Zimbabwe.