Babu Seya afunga ndoa na Katibu Tawala wa wilaya ya Muheza

Mwanamuziki Nguza Viking maarufu (Babu Seya) leo Jumamosi Septemba 7, 2019 amefunga ndoa na Bi. Desderia Haule. Ndoa hiyo imefungwa katika kanisa Katoliki la Sinza. Bi. Desderia Haule ni Katibu Tawala wa wilaya ya Muheza mkoani Tanga.