Kocha wa Liverpool, Jurgen Klopp amesema kuwa tabia ya mchezaji kushindwa kutoa pasi kwa
mchezaji mwingine ni ngumu kuitolea maamuzi hasa ukizingatia kila mmoja anatimiza wajibu wake ndani ya uwanja.
Klopp amesema kuwa kitendo ambacho alikifanya nyota wake Mohamed Salah kwa kushindwa kutoa pasi kwa Sadio Mane kilikuwa nje ya uwezo wake kwani kuna wakati mwingine Salah alikuwa akishindwa kutoa pasi na alifunga mabao yaliyoipa ushindi timu.
Ikumbuke August 31 mwaka kwenye mchezo kati ya Liverpool na Burnley Salah alishindwa kutoa pasi kwa Mane ambaye alikasirika na kulaumu kitendo hicho licha ya timu yake kushinda kwa mabao 3-0 mchezo wa Ligi Kuu England.