Mkutano wa waziri mkuu wa Somalia washambuliwa kwa bomu

Mkutano wa hadhara uliokuwa ukuhutubiwa na waziri mkuu wa Somalia, Hasan Ali Hayri uliofanyika hapo jana kusini mwa nchi hio kaika jimbo la Merka washambuliwa kwa mabomu, taarifa za kwanza zinaonyesha kwamba  watu 2 wamepoteza maisha.

Kwa mujibu wa habari kutoka katika vyanzo vya nchi hio mlipuko ulitokea katika eneo la Shabel chini katika mji wa Merka karibu kabisa na eneo ulipokuwa ukifanyika mkutano wa hadhara wakati waziri mkuu huyo akihutubia.

Habari za mwanzo zinaonyesha kwamba watu 2 wamepoteza maisha na wengine 5 wamejeruhiwa.
Mpya zaidi Nzee zaidi

Popular Items