TPB Bank yatoa vifaa tiba kwaajili ya majeruhi wa ajali ya moto



Na Edina Fidelis, Morogoro.

Kufuatia ajali ya moto iliyotokea eneo la Msamvu  manispaa ya Morogoro baada ya lori lililokuwa limebeba mafuta kulipuka  na kusabisha vifo vya watu  Zaidi ya mia moja, banki  ya posta hapa nchini [TpB]  imekabidhi vifaa tiba kwa hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Morogoro  vyenye thamani ya  shilingi milioni tatu laki tisa sabini na sita na mia tano kwa ajili ya majeruhi wa ajali hiyo ambao bado wanaendelea  na matibabu.

Akizungumza wakati wa kukabidhi vifaa tiba kwa mkuu wa wilaya ya Morogoro meneja wa banki ya posta [TpB] Eliwangu Mwangama alieleza kuwa  kama banki  imeona ipo haja  ya kutoa faida kama fungu kwa ajili ya kusaidia jamii hususani kwa upande wa afya na kuwa vifaa tiba hivyo vitasaidia kutoa huduma kwa ajili ya majeruhi wa ajali ya moto na kufidia vifaa vilivyotumika.

Mkuu wa wilaya ya Morogoro Bi Regina Chonjo alieleza kuwa vifaa tiba vilivyotolewa vitaimalisha  kitengo cha dharula cha ICU na kuwaomba  wadau mbalimbali kuweza kujitolea kwani uhitaji bado ni mkubwa wa kujiweka utayari kwa ajili ya kuimalisha huduma za kiafya katika kitengo cha maafa  kutokana na Mkoa huo kuwa katikati ya mikoa mingine.

Kwa upande wake mganga mfawidhi wa hospitali ya rufaa ya mkoa wa morogoro   Dkt. Rita Lyamuya alieleza kuwa kulikuwa na wagonjwa wa ajali ya moto ambao walikuwa kumi na nane  wakipatiwa matibabu  na hali zao wanaendelea kutengemaa na kurusiwa kurudi nyumbani  na kwa sasa wamebaki wanne wakiendelea na matibabu na kuwaomba wadau wengine kujitokeza kutoa misada mbalimbali ili kuimalisha huduma zinazotolewa katika hospitali hiyo huku mganga mkuu mkoa wa Morogoro Dkt.AR Kusirye Ukio  alieleza kuwa vifaa tiba vitasaidia kutoa huduma kama ilivyokusudiwa na kuwaomba wadau wengine kujitokeza kwani uwitaji bado mkubwa.