ATM ya maziwa yazinduliwa Moshi


Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro, Anna Mghwira amezindua ATM ya kwanza ya Maziwa Nchini katika mji wa Moshi mtaa wa chaga karibu na soko la kati

ATM hii ina uwezo wa kutoa maziwa kulingana na kiwango chako cha fedha. Unaweza pata kuanzia Tsh 50, 100, 400, 600, 1000, 2000, na kuendelea.

Mradi huu umefadhiliwa na Umoja wa Ulaya ambapo wameweka ATM 3, moja ikiwa Moshi, Hai na nyingine ipo Arusha.