Na. Rahel Nyabali, Tabora
Baadhi ya wasichana mkoani Tabora wamesema hawata kuwa nyuma kuwania nafasi za uongozi katika chaguzi za Serikali za mitaa na uchaguzi mkuu ujao wakiamini kwamba kupata uongozi kutawasiadia kuimarisha nguvu katika kukabiliana na vitendo vya ukatili wa kijinsia vinavyodaiwa kuua ndoto za maisha yao.
Wameyasema hayo wakati wakizungumza kwenye kongamano la Ajenda ya msichana ya 2019 lililoandaliwa na Shirika lisilo la kiserikali la Msichana Initiative lililofanyika Chuo cha utumishi wa umma ambapo zaidi ya wasichana elfu kutoka wilaya ya Nzega,Uyui na Tabora mjini walishiriki.
Akifungua kongamano hilo mkuu wa mkoa wa Tabora , Aggrey Mwanri amesema Serikali itaendelea kukabiliana na vitendo vya ukatili wa kijinsia ambavyo kimsingi vinadaiwa kuwaathiri Wasichana kimwili na kisaikolojia na hivyo kusababisha kuwazorotesha kifikila na kiuchumi kiuchumi ikiwemo kuwania uongozi .
Aisha uledi ni moja ya msichana walio huzulia kwenye amesema semina hiyo imewasaidia kwa kiasi kikubwa kwa wasichana kujitambua na kuweza kuwania kuwania nafasi za uongozi.
Mkurugenzi mtendaji Msichana Initiative Rebeca Ryumi amesema hii itaweza kusaidia jamii kuona ni jinsi gani msichana anaweza kuonesha na kutumia nguvu zake kama chachu ya maerndeleo na kukomesha ukatili wa kijinsia.
Aidha Mkoa wa Tabora ni miongoni mwa mikoa mitatu nchini inayoongoza kwa vitendo vya ukatili wa kijinsia ambapo Shirika la Msichana Initiative linatekeleza mpango wa kuwajengea uwezo wasichana ili iwe kichocheo kushiriki vita dhidi ya vitendo vya ukatili wa kijinsia hususani mimba na ndoa za utotoni.

