BREAKING: Yanga yamfuta kazi Mwinyi Zahera, Mrithi wake atajwa


Uongozi wa klabu ya Yanga ya jijini Dar es Salaam umemfuta kazi Kocha wake Mkuu Mwinyi Zahera.

Mbali ya kumtafuta kazi Kocha Zahera, Klabu hiyo pia imevunja benchi zima la ufundi pamoja na Kamati ya mashindano.

Kufuatia hatua hiyo Boniface Mkwasa (Master), ndiye atakua Kocha wa muda wa Klabu hiyo hadi pale itakapoamuliwa vinginevyo.