https://monetag.com/?ref_id=TTIb Nahodha wa Simba John Bocco aenda kutibiwa Afrika Kusini | Muungwana BLOG

Nahodha wa Simba John Bocco aenda kutibiwa Afrika Kusini


Nahodha wa Simba John Bocco leo ameondoka nchini kwenda Afrika Kusini kufanyiwa uchunguzi zaidi wa jeraha la misuli linalomsumbua na kumuweka nje ya dimba tangu mwanzoni mwa msimu huu.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo na klabu hiyo, Bocco amefika salama na tayari ameanza kupatiwa huduma kwenye Hospitali ya Netcare Rosebank iliyoko jijini Johannesburg.