https://monetag.com/?ref_id=TTIb Tanzania yashiriki kuadhimisha kumbukumbu ya miaka 105 baada ya vita ya kwanza ya dunia | Muungwana BLOG

Tanzania yashiriki kuadhimisha kumbukumbu ya miaka 105 baada ya vita ya kwanza ya dunia


Tanzania imeungana na Mataifa mengine duniani kuadhimisha kumbukumbu ya miaka 105 baada ya vita ya kwanza ya dunia na miaka 75 baada ya vita ya pili ya dunia maadhimisho yaliyofanyika katika eneo la makaburi ya Mashujaa yaliyoko Kijitonyama Jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) amesema ni vyema hatua za makusudi zikafanywa ili kuuimarisha na kuulinda Umoja wa Mataifa ambao amesema unahitajika sasa kuliko miaka iliyopita ili kuepuka vita,vifo na madhara yatokanayo na migogoro inayosababisha vita.