Mshambuliaji wa zamani wa Ufaransa, Thierry Henry anaamini Kylian Mbappe atatikisa zaidi katika kipindi cha miaka 20 inayokuja kwenye ulimwengu wa soka
Akiongea juu ya Mbappe, Henry ambaye anashikilia rekodi ya ufungaji bora wa muda wote wa Ufaransa, alisema anafikiria Mbappe atakuwa mchezaji ambaye wapenzi wa soka ulimwenguni watajadili juu yake kwa miaka mingi zaidi
Ufaransa leo itaongozwa na Kylian Mbappe kushuka dimbani kucheza dhidi ya Moldova katika mchezo ambao Ufaransa akishinda itakuwa imekata tiketi ya kufuzu moja kwa moja Michuano ya Euro 2020.
