Ukatili wanaofanyiwa wakina mama na Watoto katika baadhi ya maeneo hapa nchini umezifanya dini mbalimbali kuungana kwa pamoja ili kuweza kuisaidia jamii kuondoka na ukatili huo.
Kongamano hilo lililofanyika mjini Babati limeratibiwa na Shirika la Kimataifa la Norwegian Church Aid (NCA).
Wakizungumza katika Kongamano maalum la Viongozi wa dini mbalimbali mkoani Manyara zinazoundwa na Baraza kuu la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT) na Baraza kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA),Wamesema lengo lao kuu ni utekelezaji wa Malengo endelevu ifikapo mwaka 2030 katika Kutokomeza vifo vya akina mama vitokanavyo na uzazi vinavyoweza kuzuilika,Kutokomeza ukosekanaji wa taarifa na huduma za afya ya uzazi kadri ya imani za dini na kutokomeza ukatili wa kijinsia na mila potofu zinazochochea matendo ya kikatili.
TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI......USISAHAU KUSUBSCRIBE