Na Adelina Kapaya, katavi.
Takribani wanafunzi 71 Mkoa wa katavi wamegundulika na ujauzito kuanzia Januari -Novemba 2019
Takwimu hizo zimetolewa na Dawati la Jinsia na Watoto mkoa wa Katavi huku makosa ya ubakaji yakiwa 74 na makosa 9 yakiwa ni ulawitiwa.
Ikiwa ni maadhimisho ya siku 16 ya kupinga ukatili dhidi ya watoto na wanawake Dawati la Jinsia na Watoto mkoa wa katavi inatoa Elimu kwa makundi mbalimbali ili kupunguza ukatili na kutetea haki za wanawake
Mkoa wa Katavi umekua na changamoto ya Watoto kuozeshwa katika umri mdogo kuanzia umri wa miaka 11 sababu kubwa ikiwa ni wazazi kutojua umuhimu wa kumpeleka mtoto wa kike shuleni
Kutokana na hali hio imepelekea idadi kubwa ya mimba za utotoni mkoani humo na kusababisha madhara makubwa kwa wahanga ikiwemo kupoteza maisha
Dawati la jinsia na watoto limekuwa na changamoto kubwa kuhakikisha wanatokomeza mimba za utotoni kutokana na sheria inayomruhusu mtu kuolewa akiwa na miaka 14 endapo sio mwanafunzi na kwa ridhaa ya wazazi wake.
Kumekua na aÃna mbalimbali za ukatili ikiwa ni ukatili wa kingona,kiuchumi ,kimwili na kiakili. Mkoa wa katavi ameathirika zaidi na ukatili wa kingono.
Licha ya kuwepo kwa idadi kubwa ya ukatili Dawati la jinsia na Watoto kupitia uongozi wake wamejipanga kuhakikisha wanatokomeza ukatiri kwa kutoa Elimu kwa jamii.
