Waziri mkuu wa Uingereza amtaka Trump kujiweka mbali na siasa za nchi hiyo

Waziri mkuu wa Uingereza Boris Johnson amesema leo kuwa itakuwa bora iwapo rais wa marekani Donald Trump hatajihusisha na uchaguzi wa Uingereza wakati atakapofanya ziara mjini London kwa ajili ya mkutano wa NATO wiki ijayo.

Trump alijihusisha na uchaguzi huo mwezi Oktoba kwa kusema kiongozi wa upinzani wa chama cha Labour Jeremy Corbyn hatakuwa bora kwa Uingereza na kwamba Johnson anapaswa kukubaliana na kiongozi wa chama cha Brexit nchini Uingereza Nigel Farage kufanya ushirika.

Waziri mkuu Johnson amesema hata hivyo kuwa chama chake kinaweza kutimiza matakwa na wananchi wa Uingereza kujitoa kutoka Umoja wa Ulaya.

Lakini wanachama waandamizi wa chama cha Conservative wana wasi wasi kuwa Trump anaweza kuvuruga kampeni yao akiwa London, kiasi cha wiki moja tu kabla ya uchaguzi wa Desemba 12 ambao maoni ya wapiga kura yanaonesha Johnson anaweza kushinda.
Mpya zaidi Nzee zaidi

Popular Items