Akamatwa na Kilo 1.73 za dawa za kulevya akiwa amezimeza


Jumla ya kilo 1.73 ya dawa za kulevya, zikiwa katika vidonge 94, viliondolewa kutoka tumbo la raia wa Nigeria ambaye alikamatwa katika uwanja wa ndege wa Casablanca.

Raia huyo mwenye umri wa miaka 44, alikamatwa alipofika kwenye Uwanja wa ndege wa Casablanca Mohammed V mnamo Novemba 25, kwa ndege kutoka Sao Paulo nchini Brazil.

Dawa hizo ambazo zimepigwa marufuku nchini umo,zilitolewa kutoka tumbo lake katika Hospitali ya Chuo Kikuu cha Ibn Rochd, ambapo alikaa siku kadhaa chini ya uchunguzi wa matibabu