Bodi ya Utalii Rwanda kushirikiana na Klabu ya PSG kutangaza utalii


Bodi ya Utalii nchini Rwanda imesaini dili la kufanya kazi na Klabu ya PSG ya nchini Ufaransa.

Mkataba huo utawashuhudia mastaa wa PSG wakivaa Jezi zenye neno 'VISIT RWANDA' kwenye bega la kushoto kutangaza Utalii wa taifa hilo la Afrika Mashariki.

Mwaka 2018 Rwanda walisaini dili la Bilioni 102 za Kitanzania kwa miaka 3 kutangaza na Klabu ya Arsenal kupitia Jezi zao. Na walifanikiwa kuingiza kiasi cha Bilioni 202 za Kitanzania kupitia mapato ya Utalii kwa mwaka huo huo.