Mamlaka ya utafiti wa anga za mbali nchini Ethiopia watangaza kuzindua satalaiti yake ya kwanza Disemba 17.
MKurugenzi wa shirika la utafiti wa masuala ya anga za mbali nchini Ethiopia, Daktari Dr. Solomon Belay amewafahamisha wanahabari katika mahojiano aliofanya kuwa Ethiopia inajiandaa kuzindua satalaiti yake ya kwanza ifikapo Disemba 17.
Katika mahojiano yake na kituo cha habari cha Ethiopia ENA, Dr. Solomon Belay amesema kuwa satalaiti hiyo itatumiwa katika miradi ya kilimo nchini humo.
Satalaiti hiyo ETRSS-1 itarushwa nchini China na kuongozwa na kundi la wataalamu waliopo mjini Addis Ababa.
Ethiopia inaingia katika orodha ya mataifa machache barani Afrika Kusini mwa jangwa la Sahara lenye kumiliki Satalaiti.
Mataifa barani Afrika yenye kumiliki satalaiti ni Ghana , Nigeria, Afrika Kusini , Kenya na Rwanda.