Hawa ndio wachezaji 10 waliobakia kugombea tuzo ya mchezaji bora Afrika, Samatta apigwa chini


Shirikisho la soka Afrika CAF) limetangaza majina ya wachezaji 10 ambao watawania tuzo ya mchezaji bora Afrika mwaka 2019.

Kepteni wa Tanzania Mbwana Samatta ambaye aliingia katika orodha ya wachezaji 30 watakaowania tuzo hiyo tayari ametolewa.



Wachezaji waliotajwa kuwania tuzo hiyo ni Andre Onana, Hakim Ziyech, Ismail Bennacer, Kalidou Koulibaly na Mohamed Salah.
 
Wengine ni Odion Ighalo, Pierre-Emerick Aubameyang, Riyad Mahrez, Sadio Mane na Youcef Belaili.