Alichokiandika Humphrey Polepole baada ya Sumaye kukimbia Chadema


Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Humphrey Polepole amemwambia Waziri Mkuu Mstaafu Frederick Sumaye uwa alimueleza asingeweza kupata kazi ya kushauri chama chochote cha siasa kama angekuwa nje ya Chama Cha Mapinduzi.

Polepole ametoa kauli hiyi saa chache baada ya Waziri Mkuu Mstaafu Frederick Sumaye kutangaza nia yake kujiondoa ndani ya CHADEMA kwa kile alichokidai kuwa hakuna demokrasia ya kweli.

Polepole ameandika kupitia akaunti yake ya Twitter na Instagram "Mzee nilikwambia, kazi ya ushauri hutaipata ukiwa nje ya CCM wenzako wanaotushauri na tunazingatia ushauri wao kwasababu tunawaheshimu, ni wana CCM na kiitikadi tuko pamoja. Sasa umebaki bila Itikadi. Ile ni mali ya Mtu ni yake, nilikwambia mwache, ona sasa unahama mara ya pili,” ameandika Polepole.

Akitangaza uamuzi wa kujiondoa CHADEMA Waziri Mkuu Mstaafu Sumaye amesema kuwa “baada ya kutafakari kwa kina, ustaarabu unasema toka sasa hutakiwi, wako watakaosikitika nimelazimika kujiondoa CHADEMA kutoka leo hii, mimi sio Mwanachama wa CHADEMA na sijiungi na chama chochote, ila niko tayari kutumika na chama chochote”