Balozi mpya wa Tanzania nchini afrika kusini Meja Jenerali Gaudence S Milanzi amekabidhi hati ya utambulisho kwa Rais wa Afrika Kusini Mhe. Cyril Ramaphosa katika Ikulu ya nchi hiyo jijini Pretoria. Pamoja na Balozi wa Tanzania, mabalozi wengine 11 toka nchi za mbali mbali duniani nao walikabidhi hati zao za utambulisho tayari kuanza kufanya kazi katika nchi hiyo.

