Mkuu wa Wilaya ya Hai, Lengai ole Sabaya, ameeleza moja ya sababu inayochangia kurudisha nyuma maendeleo ya wilaya hiyo ni kutokana na baina ya viongozi kutonia mamoja kwenye utendaji kazi akiwemo Mbunge wa jimbo hilo Freeman Mbowe ambapo amemtaka kufanya maridhiano ndani ya chama chake , ndipo aombe maridhiano na Rais John Pombe Magufuli.
Hayo yamesemwa na Sabaya leo februari 14,2020, wakati akikabidhi pikipiki 17 kwa makatibu wa kata wa chama cha mapinduzi CCM wilayani humo.
Amesema Mbowe anapokea fedha za ruzuku za chama cha demokrasia na maendeleo (Chadema) zaidi ya shilingi 360 milioni na kwamba wanachadema hawajui zinafanyia kazi gani.
Patrick Boisaf ni Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Kilimanjaro ,amesema pikipiki hizo zitafanya Kazi ya chama kwa kurahisisha makatibu wa kata kuwatembelea wanachama pamoja na kujua shida changamoto mbalimbali zinazowakabili.