Liverpool yaendeleza ubabe Uingereza

Mshambuliaji Sadio Mane akishangilia baada ya kuifungia bao pekee Liverpool dakika ya 78 hilo likiwa bao lake la 100 England katika ushindi wa 1-0 dhidi ya Norwich kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya England leo Uwanja wa Carrow Road.

Ushindi huo unaifanya Liverpool ifikishe pointi 76 katika mchezo wa 26 ikiendelea kuongoza Ligi Kuu kwa pointi 25 zaidi ya mabingwa watetezi, Manchester City