Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika apiga marufuku mwanafunzi kusitishwa masomo



Na Adelina Ernest ,Katavi.

Mkuu wa wilaya ya Tanganyika Mkoa wa Katavi Salekhe Muhando  amepiga marufuku Mwanafunzi kusitishwa masomo yake kwa kukosa sare ya shule.

Akizungumza na wandishi wa habari amesema kuwa Mwanafunzi hatakiwi kusitishwa masomo Bali walimu wanatakiwa kuwasisitiza wazazi kununua sale hizo huku Mwanafunzi akiendelea na masomo yake

Hata hivyo amewataka wazazi na walezi kuwapeleka shule Mwanafunzi wa kidato cha kwanza na dalasa la kwanza kabla ya tarehe 15/2/2020 kwa atakae kwenda kinyume na tarehe hio hatua za kisheria zitachukuliwa . 

Baadhi ya wazazi wilayani humo wamelalamika kuwepo kwa kasumba ya baadhi ya  walimu kuwafukuza wanafunzi kwa kutokua na sale ya shule na kumuomba mkuu wa wilaya kushughulikia suala hilo.
Mpya zaidi Nzee zaidi

Popular Items