Rais Shein azungumza na uongozi wa wizara ya Kazi Uwezeshaji Wazee Wanawake na Watoto

 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed  Shein, akimsikiliza Waziri wa Kazi Uwezeshaji Wazee Wanawake na Watoto Zanzibar.Mhe. Maudline Castico, akiwasilisha  taarifa ya Utekelezaji Mpango Kazi wa Wizara yake kwa mwezi wa Julai hadi Disemba 2019 /2020, uliofanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar.

 Waziri wa Kazi Uwezeshaji Wazee Wanawake na Watoto Zanzibar. Mhe, Maudline Castico akiwasilisha Taarifa ya Utekelezaji wa Mpango Kazi  wa Wizara yake kwa mwezi  wa Julai hadi Disemba 2019 /2020, (kushoto) Katibu Mkuu Jiongozi na Katibu wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Abdulhamid Yahya Mzee na (kulia) Naibu Waziri Wizara ya Kazi Uwezeshaji Wazee Wanawake na Watoto Zanzibar. Mhe. Shadya Mohammed.

 Mkurugenzi Idara ya Mikopo Ndg. Suleiman Ali akijibu maswali yalioulizwa wakati wa mkutano huo wa Utekelezaji wa Mpango Kazi  kwa mwezi wa Julai hadi Disemba 2019 /2020, ukiongozwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein.(hayupo pichani) uliofanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar.

 Baadhi ya Maofisa  Idara mbalimbali za Wizara ya Kazi Uwezeshaji Wazee Wanawake na Watoto Zanzibar, wakifuatila mkutano huo wa uwasilishaji wa taarifa ya Utekelezaji wa Mpango Kazi kwa mwezi wa Julai hadi Disemba 2019 /2020. Uliofanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar.

 Mkurugenzi Idara ya Uwezeshaji  Ndg. Ameir Haji Sheha akijibu  masuali yalioulizwa wakati wa mkutano wa  Utekelezaji wa Mpango Kazi wa Wizara yake kwa mwezi  wa Julai hadi Disemba 2019 /2020, uliofanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, akizungumza na Uongozi wa Wizara ya Kazi Uwezeshaji Wazee Wanawake na Watoto Zanzibar, katika mkutano wa uwasilishaji taarifa ya Utekelezaji Mpango Kazi wa Wizara hiyo kwa kipindi cha mwezi  wa Julai hadi Disemba 2019 /2020, uliofanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar..(kushoto kwa Rais) Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Balozi Seif Ali Iddi na (kulia kwa Rais) Katibu Mkuu Kiongozi na Katibu wa Baraza la Mapinduzi.Dkt. Abdulhamid Yahya Mzee.