RC Ruvuma aongoza mazishi ya Wanafunzi watano waliofariki kwa kugongwa na gari

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christine Mdeme ameshiriki mazishi ya Wanafunzi watano waliofariki kwa kugongwa na gari Ruvuma.

RC Mdeme ameahidi kuendelea kumtafuta dereva aliyesababisha ajali ili achukuliwe hatua na
amehidi kusimamia matibabu ya Mtoto aliyejeruhiwa katika ajali hiyo mpaka atakapopona na kurejea shuleni.

Wanafunzi watano wa shule ya msingi Ndelenyuma,Ruvuma wamefariki Dunia na mmoja amejeruhiwa baada ya kugongwa na Land Cruiser lililokuwa likitokea Songea kwenda Madaba, Gari hilo liliacha njia na kuwagonga wanafunzi kisha likapinduka, Dereva aliyefahamika kwa jina moja la Salum ametoroka.