Samatta asababisha bao la kwanza, lakini aston villa yachapwa 3-2

MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Tanzania, Mbwana Ally Samatta amesababisha bao la kwanza la Aston Villa ikichapwa 3-2 na Tottenham Hotspur katika mchezo wa Ligi Kuu ya England leo Uwanja wa Villa Park.

Samatta aliirukia krosi ya kiungo Mholanzi, Anwar El Ghazi kujaribu kuunganishia nyavuni, lakini beki Mbelgiji Toby Alderweireld akaiwahi kujaribu kuokoa kwa bahati mbaya akajifunga kuwapa Villa bao la kuongoza dakika ya tisa tu.

Alderweireld akaisawazishia Spurs dakika ya 27, kabla ya refa Martin Atkinson kutumia msaada wa Teknolojia ya Video (VAR) kuwapa Tottenham penalti mwishoni mwa kipindi cha kwanza kufuatia Bjorn Engels kumuangusha Steven Bergwijn.