Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) tumepokea kwa masikitiko taarifa za kifo cha Katibu Mkuu wa zamani wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF), Amr Fahmy.
Tunatoa pole kwa familia ya Marehemu kutokana na msiba huo na kuwataka wawe na subira na uvumilivu kwa kuondokewa na mpendwa wao.