Kenya yatangaza kifo cha kwanza cha mgonjwa mwenye virusi vya corona

Kenya imetangaza kifo cha kwanza cha mgonwa aliyekuwa akiugua virusi vya corona.

Mwathiriwa huyo ambaye ni raia wa Kenya mwenye umri wa miaka 66 aliaga dunia nyakati za mchana katika chumba cha wagonjwa mahututi katika hospitali ya Agha Khan ambako alikua amelazwa.

Raia huyo ambaye alikua akiugua ugonjwa wa kisukari alikuwa amewasili nchini tarehe 13 mwezi Machi kutoka Afrika Kusini kupitia Swaziland.

Katika taarifa yake iliotiwa saini na waziri wa Afya Mutahi Kagwe, serikali ilisema kwamba ilipokea kwa huzuni habari za kifo cha Mkenya huyo ambaye alikuwa amekutwa na virusi hivyo baada ya kupimwa.