Watu watano watumishi wa Shirika la Reli Tanzania (TRC) wamefariki dunia katika ajali ya treni ya uokoaji iliyogongana na kiberenge kati ya stesheni ya Mwakinyumbi na Gendagenda.
Ajali hiyo imetokea jana na majeruhi mmoja anaendelea na matibabu katika hospitali ya Wilaya Korogwe.