Zaidi ya watu 11000 wamefariki kwa virusi vya corona ulimwenguni

Watu zaidi ya 11000 wamekwishafariki kutokana na virusi vya corona wamekwishafariki na kesi  270 000 ulimwenguni.

Watu 11000 wameripotiwa kufariki  ulimwenguni  na kesi 270 000   tangu kuzuka kwa janga la virusi vya corona  katika jimbo la Wuhan nchini China.

Italia ndio taifa barani Ulaya na ulimwenguni lililoathirika kwa kiasi kikubwa na virusi hivyo hatari.

Watu  wasiopungua  627 wamefariki nchini humo na kufanya idadi ya watu waliofariki kuzidi kuongezeka na kufikia watu  4032.

Kulingana na  vyanzo vya habari kutokana nchini Italia, serikali imetangaza kuchukuwa hatua  ya kupiga marufuku kutoka nje.

Wanajeshi  na maafisa walinda usalama watuhusika na  utekelezwaji wa hatua hiyo.

Nchini Uhispania  idadi ya watu ambao wamekwishafariki imefikia watu  1002 baada ya watu wengine  235 kufariki katika  muda wa masaa  235.

Mkoani Nice nchini Ufaransa  mafuruku ya kutoka nje imetanzwa  kuanzia Ijumaa.

Watu 210 wamekwishafariki nchini Marekani , hatua y a kufunga vituo vyote vya biashara mjini New YORK imetangazwa.