Kocha wa Liverpool ataja kinachombeba Salah

MOHAMED Salah Hamed Mahrous Ghaly ndio jina lake huyu nyota anayekipiga ndani ya Liverpool akiwa ni raia wa Misri na anakipiga pia kwenye timu yake ya Taifa.

Amezaliwa Juni 15,1992 ana miaka 27 ametupia jumla ya mabao 16 msimu huu ndani ya Ligi Kuu England.

Kocha Mkuu wa Liverpool, Jurgen Klopp amesema kuwa ni miongni mwa wachezaji wanaojituma ndani ya uwanja jambo linalompa nguvu ya kuendelea kupata kile anachokitaka.

"Kufuata maelekezo na kuwa na uhitaji wa kuona anachokitaka kinatokea ni miongoni mwa vitu vinavyomfanya awe hapo alipo," amesema.

Timu yake inaongoza ligi ikiwa nafasi ya kwanza baada ya kucheza mechi 29 na imejikusanyia pointi 82 kibindoni.