Wanazuoni wa kiislamu , ibada ya funga ya Ramadhani na virusi vya corona

Wanazuoni wa kiislamu watoa tamko kuhusu ibada ya funga la Ramadhani  katika kipindi cha janga la corona.

Wanazuoni wa kiislamu watoa tamko  kuhusu ibada ya funga ya mwezi mtukufu wa Rmadhani katika kipindi ambacho ulimwengu mzima umekumbwa na janga la virusi vya corona, virusi ambavyo tayari vimesababisha maafa makubwa ulimwenguni.

Wanazuoni hao wamefahamisha kuwa   janga la virusi vya corona halina athari yeyote kwa  watu ambao  hawana maradhi ya aina yeyote, wakimaanisha kuwa mtu ambae ni mzima wa afya  atalazimika kudiriki  ibada hiyo ya  funga ispokuwa kwa wale ambao watakuwa wameathirika  na hiyo ni chini ya misingi  ya uislamu.

Uislamu imeweka wazi  watu ambao  wanalazimika kufunga na wale ambao hawalazikimi kufunga kama wagonjwa.

Muungano wa wanazuoni mwa kiislamu  umefahamisha kuwa  virusi vya corona havimzuia  kufunga Radhani muislamu ambae afya yake ni salama.

Tamko hilo  limetolewa baada ya uvumi na maswali mengi kujitokeza katika jamii kuhusu ibada ya funga katika mwezi mtukufu wa Ramadhani ambao umewadia.
Mpya zaidi Nzee zaidi

Popular Items