Brazil yagomea kusitisha matumizi ya hydroxychloroquine kutibu corona

Nchi ya Brazil imesema haitositisha matumizi ya dawa ya hydroxychloroquine kutibu ugonjwa wa covid-19 hata baada ya WHO kuonya madhara ya dawa hio kiafya ambayo awali ilitumika kutibu ugonjwa wa malaria.

Brazil imeripoti vifo zaidi ya 807 ndani ya masaa 24 yaliyopita ikiwa na jumla ya vifo 23,473 na visa 374,898. Brazil sasa inashikilia nafasi ya pili kwa Nchi zilizoathirika na virusi vya corona ikiongozwa na Marekani.