Na John
Walter-Manyara
Madaktari na
wahudumu katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Manyara wameomba wahisani, wafadhili
na watu mbalimbali kuwasaidia vifaa vya kujikinga na maambukizi ya virusi vya
corona.
Wametoa ombi hilo wakati wakipokea msaada wa vitakasa mikono vifaa vilivyotolewa na Shirika la kuhudumia
Viwanda (SIDO) Mkoa wa Manyara.
Akizungumza
kwa niaba ya mganga mfawidhi wa hospitali hiyo, Daktari wa Magonjwa ya ndani
Dr. Yesige Mutwajaa, alisema kwa sasa
wana uhaba wa vifaa Kinga hivyo kwa mtu yeyote,kampuni au Taasisi iwasaidie
kupata vifaa vitakavyoweza kuwasaidia kwenye mazingira yao ya kazi.
Dr. Yesige alisema kuwa serikali peke yake haitaweza
kufanya kila kitu hivyo wadau wanapojitokeza kusaidia vifaa kinga itarahisisha
mapambano na kuvishinda virusi vya corona kwa pamoja.
Meneja wa
SIDO Mkoa wa Manyara Abel Mapunda akikabidhi vifaa hivyo, amesema wameamua
kutoa msaada wa vifaa hivyo ili viweze kuwasaida wataalamu wa afya na wahudumu
katika hospitali hiyo katika kuwasaidia
kujikinga na ugonjwa huo ikizingatiwa kuwa wanawahudumia wagonjwa wengi
wakiwemo wa Corona.
Mapunda
alisema kuwa utoaji wa msaada huo ni katika jitihada za kuendelea kukabiliana na
ugonjwa wa homa ya Mapafu-Corona.