Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Pius Msekwa, amesema kuwa CHADEMA wako sahihi kuwafukuza wanachama wake ambao wameenda kinyume na taratibu zao kwa mujibu wa katiba ya chama hicho.
"Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kiko sahihi kuwafukuza wabunge wake kutoka kwenye chama hicho, hivyo mamlaka hayo wanayo kwa mujibu wa katiba ya chama" amesema Mzee Msekwa.
Hivi karibuni CHADEMA kupitia kwa Katibu wa chama hicho John Mnyika, kiliwafukuza uanachama wabunge wake wanne, akiwemo David Silinde, Anthony Komu, Wilfred Lwakatare na Joseph Selasini, baada ya kukiuka maagizo na maelekezo ya chama.
"Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kiko sahihi kuwafukuza wabunge wake kutoka kwenye chama hicho, hivyo mamlaka hayo wanayo kwa mujibu wa katiba ya chama" amesema Mzee Msekwa.
Hivi karibuni CHADEMA kupitia kwa Katibu wa chama hicho John Mnyika, kiliwafukuza uanachama wabunge wake wanne, akiwemo David Silinde, Anthony Komu, Wilfred Lwakatare na Joseph Selasini, baada ya kukiuka maagizo na maelekezo ya chama.
