Waziri wa Kazi Uwezeshaji Wazee Wanawake na Watoto Dk Moudline Cyrus Castico ameitaka Bodi ya Mfuko wa Uwezeshaji Wananchi Ki uchumi kufanyakazi zake kwa ushirikiano, uaminifu na kujituma ili Mfuko huo uwe endelevu .
Hayo ameyaeleza wakati akizindua Bodi hiyo huko kwenye ukumbi wa
Wizara yake Mwanakwerekwe wilaya ya Magharib B’ Unguja.
Amesema kwa kufanya hivyo Mfuko huo utafikia malengo
yake na kutoa huduma za Mikopo kwa Wajasiriamali na Wananchi kwa ujumla.
Dr. Moudline amesema Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imeanzisha
Mfuko huo ilii Wananchi wake wakopeshwe ili kutunisha fedha za miradi yao
wanayoiendesha ili kuweza kujiajiri na kujipunguzia umaskini.
“Mahitaji yamekua makubwa maombi ya Mikopo yanapokelewa kila siku
,hivyo mshirikiane na Uongozi wa Wizara ili kupata mbinu za pamoja za
kutunisha fedha kupitia Mfuko huo “Ameisisitiza bodi hiyo .
Halkadhalika ameitaka Bodi kujenga tabia ya kutembelea wateja wa
Mfuko huo waliopo Mjini na Vijijini Unguja na Pemba ili kuona
maendeleo yao katika miradi mbalimbali wanayoiendesha pamoja na
kuhamasisha wananchi kutumia huduma za Mfuko huo.
Bodi hiyo ambayo ina wajimbe Sita Mwenyekiti wake
ni Bi.Amina Ismail Kanduru na wajumbe ni Bw. Ali Aboud Mzee ,
Bi.Fatma Iddi Ali, MHE. Ahmada Yahya Abdulwakil , Bw. Suleiman Haji
Ali Bi. Mwanahija Almasi Ali . na Bi. Abeida Rashid
Abdalla.
