Mwnamke aliyefumaniwa na mume wa mtu na kupigwa adai kuibiwa laki 9

Mwanamke Vena Kimaro mkazi wa kata ya Msaranga katika manispaa ya Moshi ambaye video yake imesambaa kwenye mitandao ya kijamii akionekana kupigwa na Mwanamke mwenzake kwa kile kinachotajwa kufumaniwa akifanya mapenzi na mume wa mtu ameeleza kuwa alikutana na mwanaume huyo kuzungumzia mipango ya kushirikiana kibiashara.

Venna amedai alichukuliwa fedha zake zaidi ya Tsh.Laki tisa na Mwanamke huyo aliyempiga, Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Anna Mgwhira amefika nyumbani kwa Mwanamke huyo na kusema atahakikisha anapata matibabu na taratibu nyingine za kisheria zitafuata.