PSG yamtengea dau Mauro Icardi

Klabu ya Paris Saint-Germain (PSG) wameanza kutoa ofa ya £44.7m (€50m) ikijumuishwa na kiasi cha nyongeza cha £8.9m (€10m) kwaajili ya kumsajili jumla mshambuliaji Mauro Icardi kutoka klabu ya Inter Milan.

Icardi amekua kwa mkopo PSG tangia kipindi cha kiangazi kilichopita kwa dili ambalo lilijumuisha kipengele cha kumnunua jumla kwa kiasi cha £62.7m (€70m).