VIDEO: Mtoto amuua mama yake kwa kumkatakata na shoka kisha kunywa damu yake


Kijana anayedhaniwa kuwa na matatizo ya akili, Daniel Emanuel (32) mkazi wa Sakila Chini wilaya ya Arumeru Mkoani Arusha amemuua kikatili mama yake mzazi kwa kumkata vipande kwa shoka na kutenganisha kiwiliwili kisha kunywa damu yake.

Tukio hilo la kusikitisha limetokea Jana majira ya saa 9 alasiri nyumbani kwa marehemu katika kijiji cha Sakila chini wilaya ya Arumeru,mkoani hapa. 

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo Kamanda wa polisi jiji Arusha, Jonathan Shanna amemtaja marehemu kuwa ni Eliamulika Emanuel mwenye umri wa miaka 79 mkazi wa Sakila chini wilayani humo ambaye alikuwa akiishi jirani na mtuhumiwa ambaye ni mama yake.

TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI.......USISAHAU KUSUBSCRIBE