F Watu 120 wamekamatwa katika maandamano Hong Kong | Muungwana BLOG
https://c2p.cleverwebserver.com/dashboard/6a0bec4b-79ba-11ef-ad2b-06f0639468d1

Watu 120 wamekamatwa katika maandamano Hong Kong


Watu  120 wameripotia kukamatwa Hong Kong katika maandamano ambayo yameanza upya baada ya kuonekana kuwa janga la virusi vya corona sio tena   tishio katika jamii.

Waandamanajji wamemiminika mabarabarani  kupinga  mpango wa sheria mpya kutoka China ambayo  inadiwa kuingilia  masuala ya ndani ya Hong Kong.

Katika maandamano hayo, waandamanaji  zaidi ya  120 wameripotiwa kukamatwa.
Mamia ya waandamanaji wamekusanyika mjini kati Causeway Bay wakiwa wamevalia mavasi meusi kama ishara ya kupinga msuada huo wa sheria.

Waandamanaji wamesikika wakitoa matamshi dhidi ya serikali.

Jeshi la  kutuliza ghasia  lmetumia mabomu ya kusababisha kutokwa na machozi kuwatawanya waandamanaji hao.

Miongoni mwa watu waliokamatwa, amekamatwa piia mwanaharakati maarufu anaefahamika kwa jina la Tam Kakchi.

Askari polisi wanne pia wameripotiwa kujeruhiwa katika maandamano hayo.