RC Makonda atuma salamu kwa Mnyika Kibamba


"Mimi ndo kijana ukinisema sijali kabisa,huko Twitter nyie semeni, chambueni mpaka mchoke mimi nachojua ni kuwa kazi zinafanyika na maendeleo yanaonekana wazi wazi, nawapa salamu kule kwa Katibu wao CHADEMA, John Mnyika kesho naanza ziara wajipange maana najua hakuna alichofanya" Rc Paulo Makonda RC Paul Makonda

"Wakati naanza ziara vijana wa pale mtaa wa Ufipa wamenitafuta wanaomba niwasaidie kulipa pango la ofisi yao Makao Makuu pale, CHADEMA wanadaiwa kodi ya miezi sita kama naongopa waweke risiti hadharani tuone kama wamelipa kweli kuanzia January mwaka huu, Mwenyekiti wa Chama Kinondoni ikitokea wamefukuzwa wape ofisi yako ile ya zamani wasije sema oooh tumefukuzwa" RC Paul Makonda