Wizara ya Afya imerekodi visa vipya 40 vya COVID19 nchini humo na idadi ya maambukizi hadi sasa ni 457, Wagonjwa wapya wote ni raia wa Uganda
Wagonjwa 23 kati yao ni madereva wa malori waliotokea Sudan Kusini (20), Tanzania (2), na mmoja aliyeingia nchini humo kupitia mpaka wa Padea, na wengine ni watu waliokuwa karibu na wagonjwa ambao tayari wamethibitishwa
Wizara pia imesema madereva 31 ambao ni Wakenya-19, Watanzania-11 na mmoja kutoka Eritrea walikutwa na maambukizi ya #CoronaVirus na kurudishwa katika nchi zao
