Watu tisa wafariki dunia katika ajali ya boti Kigoma

WATU tisa wamefariki  baada ya boti la abiria kuzama  katika ziwa Tanganyika, Kamanda wa polisi mkoa wa Kigoma Kamishna msaidizi MARTIN  OTTIENO amethibitisha.

Kamanda Otieno amesema ajali hiyo imetokea  katika eneo la Rasini na kusema kuwa Boti  iitwalo "Mv Nzeimana"  inalofanya safari zake kati ya Kijiji cha Sibwesa na Ikola  limezama  ikiwa na abiria 60, ambapo abiria 51 wameokolewa.

Aidha Kamanda OTTIENO amesema chanzo cha ajali hiyo ni upepo mkali uliosababisha boti hilo kukosa muelekeo na hatimaye kupinduka.
Mpya zaidi Nzee zaidi

Popular Items