https://monetag.com/?ref_id=TTIb Yanga yaweka historia ya aina yake, yasaini mkataba na La Liga | Muungwana BLOG

Yanga yaweka historia ya aina yake, yasaini mkataba na La Liga

Kutokana na janga la Corona viongozi wa La Liga na wale wa Sevilla wameshindwa kuhudhuria tukio la kusaini mkataba wa mabadiliko ya mfumo wa uendeshaji la kihistoria iliyofanyika pale Serena Hotel.

Hata hivyo viongozi hao wametuma video clip wakielezea uzuru wao na kueleza mpango kazi wao nini watakifanya kuhakikisha Yanga SC inafanikiwa kisha mkurugenzi wa La Liga akasaini mkataba na kuutuma kisha Yanga SC kuupokea, Mshindo Msolla na Eng Hersi Said wameusaini na kukamilisha zoezi!

Rais mstaafu wa awamu ya nne Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete ambaye alikuwa mgeni rasmi katika tukio hilo amepongeza jitihada hizo zinazofanywa na viongozi hao hivyo amewataka kuendelea na uimarishaji katika sekta ya michezo.

“Niwapongeze kwa hili la leo, matamanio ya uendeshaji kwa Yanga ni ya muda mrefu toka kwa Castro Mponela. .alipokuja na Yanga kampuni , la pili alipokuwa Yusuf Manji alipokuja na dhana ya kukodisha hili litakuwa la tatu mengine yalikuwa kubadilisha katiba”. Amesema Dkt.Kikwete.