Viongozi na wanachama wa Chadema wafurika uwanja wa ndege kumpokea Tundu Lissu




Viongozi na wanachama wa Chadema wafurika kumpokea Tundu Lissu katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere.

Joseph Mbilinyi ,mbunge amesema "Unaachaje kuja kumpokea mtu aliyepigwa risasi 16 na bado yuko hai, huyo ni mbeba maono lazima tumpokee".


"Nimekuja kushuhudia miujiza ya kupona kwa Lissu, sisi tuliokuwa Dodoma tuliona jinsi alivyokuwa ndio maana tumekuja kumshuhudia shujaa", Joseph Haule mbunge wa chama hicho.

Mabango mengi yakiwa yameandikwa karibu kiongozi yalikuwa yamebebwa na wanachama huku wakiwa wamevalia sare.