Drogba 'atia nia' kuongoza soka Ivory Coast


Mshambuliaji wa zamani wa Chelsea Didier Drogba ametuma rasmi maombi ya kukiongoza chama cha soka cha nchi yake Ivory Coast Football Federation (FIF).

Drogba alirejesha fomu za maombi yake jana Jumapili na kulakiwa na maelfu ya mashabiki wake.

Uchaguzi wa FIF unatarajiwa kufanyika baadae mwezi ujao na Drogba ni miongoni mwa wagombea wanne waliojitokeza katika kinyang'anyiro hicho.


Mpya zaidi Nzee zaidi

Popular Items

Kilimo cha Bamia